Saturday, 26 April 2014

EVIL SEX SEHEMU YA PILI (2) NI SIMULIZI YA KUSISIMUA HISIA ZAKO SOMA HAPA KWA UNDANI ZAID UBURUDIKE....

                                                                EVIL SEX SEHEMU YA PILI (2)

Edd akastukia akiguswa begani akageuka na kukutana na Janet ambaye ni mpenzi wake tangu walipoanza chuo

"Eddy mbona nilikuwa nakupigia simu hupokei?"

"Muda mwingine si ninakuwambia ninakuwa darasani sasa nitapokeaje?"

"Ok leo nataka tutoke pamoja usiku"

"Bwana mimi nitakuwa najisomea"

"Eddy hivi unajua siku hizi umebadilika sana kwanza unanijibu upendavyo,hunijali na wala nisikufiche story zako zote nazijua"

Janet alizungumza kwa hasira huku machozi yakimlenga lenga

"Kama umeijua sijui umejua story zangu basi zichukue na uziandikie kitabu uuze basi"

Eddy akaanza kuondoka Janet akapiga hatua na kumvuta tishet yake kwa nyuma Eddy akageuka kwa hasira

"Nimesema niachie wewe mwanamke kabla sijakufanya kitu kibaya"

"Eddy leo hii ndio unazungumza hivyo baada ya kuutoa usichana wangu ndio umekuwa jeuri si ndio"

"Kwahiyo unahitaji nikurudishie huo usichana wako...kesho nitakwenda kukununulia wa kichina nikuwekee"

Janet akampiga Eddy kofi la shavu la kushoto jambo lililozidi kumkasirisha Eddy

"Sikia wewe usitake nikufanyie kitu ambacho sijapanga kukufanyia nitaiharibu sura yako hiyo"

Eddy akandoka na kumuacha Janet akiwa analia kwa uchungu,Janet akajikokota taratibu hadi hostel anayoishi na kujilaza kitandani huku akilia kwa uchungu

Simu ya Eddy ikaita na namba ngeni ndio inapiga kwa haraka bila kujiuliza akapokea

"Mambo shem"
Ni sauti ya Maria rafiki wa Janet ilizungumza na kusababisha tabasamu la Eddy kupotea usoni

"Pouwa"

"Shem umemfanya nini Janet?"

"Ngoja nitakupigia nipo bize"

Eddy akakata simu na namba za Janet na Maria akaziweka kwenye black list kabla hajairudisha mfukoni simu ikaita na namba ngeni,akapokea na kusikilizia

"Hallow Eddy"

Sauti nzuri ya kike ilisikika

"Pouwa nani mwenzangu"

"Best yako yule uliyenipa namba jioni.Uko wapi?"

"Hostel wewe je"

"Njo basi hapa ZKY Hotel tupige mastory"

"Powa dakika kumi nitakuwa hapo"

Eddy akakata simu kwa furaha na kujiandaa haraka,akakodi tax hadi ZKY alipoambiwa kwa bahati nzuri wakaonana

ITAENDELEA..........!!!!!

No comments:

Post a Comment